|  Home  |  About Us  |  Information Center  |  News & Events  |  Publications  |  Where we are  |  Site Map  |  Contact us  | 

KARI T A A R I F A


Toleo la Taasisi ya Utafiti wa Kilimo ya Kenya, Julai 1997. Nambari 1

Mtama wasaidia kutosheleza akiba ya chakula nchini

Katika sehemu zenye uhaba wa mvua nchini Kenya, wengi wanantambua mtama una nafasi bora zaidi kutosheleza akiba ya chakula. Mtama ni mmea wa kiasili nchini Kenya.

Hata hivyo, ulipungua dhamana yake kwa wakulima kwenye sehemu ambazo mahindi yalipendekezwa kuwa mmea na chakula bora zaidi. Kwa wakati huu, wakulima wengi wanazidi kutambua kuwa mtama ndio unaweza kufanya vizuri katika sehemu ambazo mahindi yameshindwa kustawi.

Katika wilaya ya Machakos ambayo ilikumbwa na ukame mwaka wa 1996, wakulima waliopanda mtama walipata mavuno mazuri ikilinganishwa na mavuno ya wale waliopanda mahindi. Pius Mwania na mke wake Jane wanatoa ushahidi wa tukio hili. "Wale waliopanda mahindi hawakuvuna chochote", alisema Bi. Mwania.

Wakiwa baadhi ya wakulima wengi wilayani Machakos, Bwana na Bi. Mwania, hupenda mtama aina ya KARI/Mtama-1 ulioendelezwa na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo nchini Kenya - KARI. Mtama huu ulitolewa mwaka wa 1994 na umevutia wakulima nchini; wengi husema kuwa ni mtamu na unaweza kutumika kwa kupika ugali wa ngano ili kuoka mikate na chapati. Aina ya mtama uliyo na mbegu za rangi ya maji kunde unaojulikana kama Seredo (na ambao pia uliendelezwa katika vituo vya utafiti vya KARI, na hutumika kwa kupika ugali na uji. Kampuni maarufu ya kuoka mikate, Makatiat Ltd., hushirikana na KARI kwa utumiaji wa KARI/Mtama-1 kwa kuoka mikate (asili mia 15 ya unga wa mtama na 85 unga wa ngano), keki na biskuiti (asili mia 50 unga wa mtama na 50 unga wa ngano).

Huko magharibi mwa Kenya na mkoa wa Nyanza, mtama hutumika sana kama chakula cha kuku. Wakulima katika sehemu hii husema kwamba kuku wa kienyeji hutaga sana wakilishwa mtama. Ugali wa mtama hudhaminiwa sana katika sehemu hii haswa ukichanganywa na unga wa mihogo.

Kufuatia ombi la viongozi katika wilaya ya Baringo wakitaka usaidizi wa mimea ambayo huweza kustawi katika sehemu zinazokumbwa na ukame mara kwa mara, KARI ilianzilisha mradi wa ujamaa wa kiumarisha ukuzaji wa mtama huko Cheplambus, sehemu yenye mabonde na milima. Ukosefu wa mvua katika sehemu hii husababisha uharibifu wa mahindi kabla hayajakomaa.

Mtama aina ya KARI/Mtama-1 ulijaribiwa katika wilaya ya Baringo ili kutosheleza akiba ya chakula na pia kama kielelezo cha hali iliyoimarishwa katika mbinu za kutunza mimea na kuzalisha mbegu zaidi. Mradi huu ulianzishwa mwaka wa 1992 na tangu wakati huo, eneo linalokuzwa mtama limepanuka na mazao kwa wakulima yakaongezeka.

Mmoja wa wakulima wanaoshiriki kwennye mradi huu ni Bwana Charles Rutto mwenye umri wa mika 38 na jamii ya watoto 6. Bwana Rutto amekuza mtama kwa miaka 5. Amepanda ekari 5 katika shamba lake na 5 katika shamba la kukodisha. Yeye huamini kuwa sehemu hii ya Baringo imefaidika zaidi kutokana na juhudi za mradi huu na hivi karibuni itajitosheleza kwa chakula. Chakula cha mchanyiko wa mtama na maharagwe huliwa na jamii nyingi na wameridhika kwamba ni chakula kitamu kilicho maarufu.

Bwana Rutto na wakulima wengine wameanzisha chama ushirika wa wakulima kitwacho EMKWEN Farmers Society kinacho wapatia huduma za kupima uzito wa mtama, uhifadhi, ununuzi wa magunia na uchukuzi.

Mkulima mwingine asili wa mtama ni Bwana Wilson Kipng'ok anaetambuliwa kwa uhodari wa kutunza mtama. Shamba lake limetumika kama uwanja wa kuonyesha na kuelezea wakulima mbinu halisi za kutunza mashamba, kupanda mbegu, matumizi ya mbolea, kupanda mtama na mbaazi kwa kutumia mbinu za kilimo mseto na kupalilia. Bwana kipng'dk hutumia jembe la kukokotwa na ng'ombe kuchimba mitaro ya kuhifadhi udongo na maji shambani.

Ndege husababisha hasara kwa wakulima wa mtama katika sehemu nyingi kwa wakulima wa mtama katikja sehemu nyingi nchini. Njia moja inayotumiwa na wakulima kwa kufungwa kwenye vikingi vilivyozunguka shamba. Mikebe hiyo huunganishwa kwa kamba ambazo zikivutwa husababisha makelele yanyowafukuza ndege

KARI imedhihirisha manufaa ya KARI/Mtama -1 kwa kuchanganya na nafaka nyingine (k.m. wimbi wa kiasili, wimbi aina ya Pearl na ngano) kwa kampuni zinazosaga unga nchini kama KEN-UJI Products wilayani Meru na Elina ASAL Food Products Wilayani Embu. Bw. Stephen Marete wa KEN-UJI hununua mtama kwa wingi (gunia 500 na zaidi) kutoka kwa wakulima katika wilaya ya Tharaka Nithi.

Vituo vya KARI huko Perkerra, Katumani, Kisii, Embu na Kakamega vinashirikiana na vikundi vya wakulima vinavyokuza mtama. KARI inanuia kuwapa wakulima wengi wanaoweza kunufaika katika sehemu hizo mbegu na habari za ukuzaji wa KARI/Mtama-1 kupitia kwa vituo vyake vya utafiti. Mmea huu hufanya vizuri katika sehemu zenye miinuko ya kati ya nita 50 hadi 1700 juu ya usawa wa bahari, na zenye mvua ya kiasi cha milimita 300 au zaidi. Sehemu zinazopendekezwa kwa ukuzaji wa KARI/Mtama-1 zinajumuisha mikoa ya Mashariki, Magharibi, Nyanza na Bonde la Ufa (sehemu kama Baringo, Turkana, Pokot Magharibi, Nakuru) na sehemu kadhaa katika mkoa wa Kaskazini Mashariki. KARI imenunua mbegu kutoka kwa wakulima na kuzisambaza katika vituo vya utafiti, kwa maafisa wa kilimo wilayani na kwa vikundi vingine vinavyoweza kunufaishwa na KARI/Mtama

WIMBI WAJITOKEZA

Wimbi ni mmea ambao umekuzwa kwa muda mrefu barani Africa. Wimbi una uwezo wa kustawi katika sehemu zenye uhaba wa mvua ndiyo sababu umejumlishwa na mimea mingine ambayo inasaidia kutosheleza akiba ya chakula nchini Kenya.

Umaarufu wa wimbi ulionekana wazi wakati wa misimu ya kupanda ya mwaka wa 1996. Huko wilayani Kakamega, duka la kuuzia mbegu la kampuni ya Kenya Seed Company liliuza mbegu zaidi ya maradufu ya zile zilizouzwa mwaka wa 1995. Afisa mmoja wa kampuni hii alisema kwamba wakulima wengi walinunua mbegu za wimbi kwa sababu mapato ya mahindi ya mwaka uliopita hayakuwa mazuri. Baadhi ya mbegu za wimbi ziliuziwa miradi ya ukulima ya vijana na shule za upili.

Wanasayansi wa KARI wameutia wimbi maanani zaidi. Kituo cha utafiti cha Kakamega kilianzisha mradi mkubwa wa kuzalisha wimbi. Mradi huu tayari umefaidika kwa kupokea mbegu kutoka sehemu mbali mbali nchini ambazo zinafanyiwa utafiti. Kutokana na matokeoya uchunguzi wa mbegu hizi, KARI imetoa aina kadhaa za mbegu za wimbi kama, P224 iliyo maarufu, na KAT/FM-1.

Wimbi hukomaa na kutoa mazao ya kuridhisha katika sehemu ambazo mahindi hayastawi. Licha yakuwa wimbi haukuzwi kwa wingi kama mtama, ni chakula chenye manufaa ambacho kina madini muhimu kama calcium. Jamii za mapato ya juu zinazidi kuzoe chakula cha wimbi na kuna majribio ya kujumlisha wimbi kwenye baadhi ya vyakula vya watoto. Ugali na uji uliopikwa na unga wa wimbi unazidi kuwa maarufu kote nchini. Juhudi za kuvumbua kinga ya kuzuia wadudu na kwekwe wanaodhuru wimbi na hata inzi wanaovamia mimea michanga zazidi kufanyiwa uchunguzi katika kituo cha Kakamega. KARI imechapisha matokeo ya mbinu za kisasa za upanzi, matumizi ya mbolea na ukuzaji wa wimbi.

Watafiti wa KARI wanashugulika kuendeleza wimbi aina ya Pearl ambao hukomaa mapema na hivyo kuepuka misimu ya ukame.

SHUKRANI
Taarifa hii inayoendeleza matokeo ya utafiti wa kilimo imedhaminiwa na Idara ya Maendeleo ya Kimataifa ya Amerika (USAID) kwa jukumu la Mradi wa KARI wa Utafiti wa Kilimo Nchini (NARP)

Editor: Dr. J. O. Mugah
Layout: Ms. Grace Kimani
Fore more info.
Director, KARI
P. O. Box 57811
Nairobi, Kenya
Tel. 254-02-583301-20
email: Director@kari.org
email: Resource.center@kari.org

 


© Copyright Kenya Agricultural Research Institute. All rights reserved